languageIcon
search
search
brightness_1 Ni katika Suna kusalimu.

Na hoja ya Suna hii ni nyingi mno. Miongoni mwa hoja hizo ni: Hadithi ya Abuhuraira -RAA- akinukuliwa kusema kwamba, Mtume-SAW- amesema kuwa: “Haki za Muislamu kwa Muislamu (mwenzake) ni sita. Mtume aliulizwa: Ni zipi haki hizo ewe Mtume wa Allah? Mtume akasema: Ukikutana naye msalamie, na akikualika muitikie, na akikutaka ushauri mshauri, na akipiga chafya akamhimidi Allah (yaani akasema Alhamdulillaah), muombee Rehema (Mwambie: Yarhamukallaahu), na akiugua mtembelee, na akifa sindikiza jeneza lake”. Imepokewa na Muslim kwa nambari (2162).

-Ama kujibu Salamu ni: wajibu. Na hoja juu ya hili ni:

Kauli ya Allah Mtukufu isemayo kuwa: {Na mtakapoamkiwa kwa maamkizi yoyote, itikieni kwa maamkizi yaliyo mazuri zaidi kuliko hayo au yarudisheni hayo hayo. Hakika, Allah daima ni Mwenye kuhesabu kila kitu}. (Sura Annisaa: 86).

Na asili katika amri ni lazima, madamu amri hiyo haijaondolewa na cha kuiondoa (katika ulazima). Wanazuoni wengi wamenukulu makubaliano juu ya wajibu wa kujibu Salamu. Miongoni mwa wanazuoni hao ni Ibnihazmi, Ibniabdulbari, Sheikh Taqiyyudiin na wengine – Allah awarehemu wote-. Angalia: Al-aadaab Ash-shar-iyya (1/356), chapisho la Mu-assasaturrisaala.

-Na tamko bora na kamilifu mno la kusalimu na kujibu Salamu ni: (Assalaamu Alaykum Warahmatullaahi Wabarakaatuh = Amani iwe kwenu na rehema za Allah na Baraka zake). Tamko hii ndio salamu bora zaidi na timilifu zaidi.

Ibnulqayyim –Allah amrehemu- amesema kuwa: “Na muongozo wa Mtume -SAW- ulikuwa kuishia Salamu mpaka: (Wabarakatuh)”. Angalia: Zaadul Ma’ad (417/2).

Na kutangaza Salamu sio kwamba ni Suna tu, lakini pia ni Suna iliyotiwa ushawishi kwamba ina fadhila kubwa, kwa mujibu wa Hadithi ya Abuhurara -RAA- akinukuliwa kusema kuwa, Mtume wa Allah-SAW- amesema kwamba: “Nina apa kwa (Allah) ambaye nafsi yangu iko mkononi mwake, hamtaingia Peponi hadi muamini. Na hamuwezi kuamini hadi mpendane. Je, nikufahamisheni jambo ambalo mtakapolifanya mtapendana? Tangazeni Salamu baina yenu”. Imepokewa na Muslim kwa nambari (54).

 

brightness_1 NI KATIKA SUNA KUSALIMIA WAKATI WA KUINGIA NYUMBANI.

Na hii inaingia katika ujumla wa kusalimia. Na hayo ni baada ya kupiga mswaki, kwa sababu kupiga mswaki unapoingia nyumbani ni Suna. Hii ndio sehemu ya nne katika sehemu ambazo Suna ya kupiga mswaki inasisitizwa. Sehemu hiyo ni: Wakati wa kuingia nyumbani, kwa mujibu wa Hadithi ya Bi Aisha –RAA- katika mapokezi ya Muslim. Aisha amenukuliwa kusema kuwa: “Mtume –SAW- alikuwa anapoingia nyumbani kwake anaanza kwa kupiga mswaki”. Imepokewa na Muslim kwa nambari (254).  Mtume alikuwa akianza kuingia nyumbani kwake kwa kupiga mswaki kisha huingia na kuwasalamia waliomo humo. Baadhi ya Wanazuoni wamesema kuwa: Ni katika Suna kusalimia unapoingia kwenye nyumba yoyote, hata kama ndani ya nyumba hiyo hakuna mtu yeyote, kwa mujibu wa kauli ya Allah kwamba: {Na mtakapoingia majumbani salimianeni (kama kuna watu, na kama hakuna watu jisalimieni wenyewe); maamkizi kutoka kwa Allah, yenye Baraka, mazuri. Kama hivyo Allah anakubainishieni Aya ili mpate kutia akilini}. Sura Annuur, aya 61.

Ibnihajar- Allah amrehemu amesema kuwa: “Na inaingia katika ujumla wa kutangaza Salamu kwa mtu mwenye kuingia sehemu ambayo hakuna mtu yeyote, kwa mujibu wa kauli ya Aliyetukuka kwamba: {Na mtakapoingia majumbani toleaneni salamu (kama kuna watu, na kama hakuna watu jisalimieni wenyewe)}. Angalia: Fat-hulbaariy, Hadithi (6235), mlango wa kutoa Salamu.

Faida: Imepatikana kutoka katika maelezo yaliyopita kwamba kuna Suna za aina tatu wakati wa kuingia ndani nyumba:

Ya kwanza: Kutaja jina la Allah, na hasa usiku.

Kwa mujibu wa Hadithi ya Jabir bin Abdallah -RAA- kwamba, alimusikia Mtume - SAW- akisema kuwa: “Mtu anapoingia nyumbani kwake, na akamtaja Allah wakati wa kuingia kwake, na wakati wa kula kwake, shetani husema (kuwaambia wenzake): Hakuna pa kulala leo wala chakula cha jioni. Na mtu anapoingia (nyumbani kwake) na hukumtaja Allah, shetani husema (kuwaambia wenzake): Mmepata pa kulala. Na kama hakumtaja Allah wakati wa kula kwake, shetani husema (kuwaambia wenzake): mmepata pa kulala, na chakula cha jioni”. Imepokewa na Muslim (2018).

Ya pili: Kupiga mswaki, kwa mujibu wa Hadithi ya Bibi Aisha –RAA- iliyotangulia kutajwa hapo nyuma.

Tatu: Kuwasalimia walioko nyumbani.