languageIcon
search
search
brightness_1 DUA ILIYOTHIBITI BAADA YA UDHU.

Imenukuliwa kwa Umar –Allah amridhie- akisema kuwa, amesema Mtume wa Allah–SAW- kwamba: “Hakuna yeyote kati yenu anayetawadha akautimiza vilivyo Udhuu wake, kisha akasema: “Nashuhudia ya kwamba hapana mwenye haki ya kuabudiwa isipokuwa Allah tu, na kwamba Muhammad ni Mja Wa Allah na Mtume Wake, (Ash-hadu Allaa ilaaha illa-llaah, Wa-ash-hadu Anna Muhammadan Abdullaahi Warasuuluhu) isipokuwa atafunguliwa milango minane ya pepo aingie kupitia mlango wowote autakao”. Imepokewa na Muslim kwa nambari (234).

Au Dua iliyokuja katika Hadithi ya Abusaid–Allah amridhie- ikihusishwa na Mtume kwamba “Mwenye kutawadha kisha akamaliza Udhu wake na akasema: Sub-hanakallahumma Wabihamdik, Ash-hadu Allaa Ilaaha Illaa Anta, Astaghfiruka Wa-atuubu Ilayika, (Utukufu na sifa njema zote ni zako. Nashuhudia kuwa hapana apasaye kuabudiwa kwa haki ila wewe tu. Naomba msamaha wako na natubu kwako), Allah hupiga muhuri na kuwekwa lakiri, kisha ikanyanyuliwa na kuwekwa chini ya Arshi na haitavunjwa lakiri hiyo mpaka siku ya Kiyama”.  Imepokeleawa na Nasai katika Matendo ya Usiku na Mchana. (Ukurasa 147). Pia ameipokea Hakim (1/752) na Ibnihajar – Allah amrehemu-amesema kuwa orodha ya wapokezi wake ni sahihi. Angalia Nataa-ijul-afkaar, (1/246). Ameendelea kubainisha kuwa, kama sio sahihi kuihusisha kwa Mtume, basi imehusishwa kwa Swahaba. Hilo halina tatizo, kwa sababu jambo hilo linachukua hukumu ya kuhusishwa kwa Mtume, kwakuwa ni miongoni mwa mambo ambayo rai ya mtu haina nafasi katika mambo hayo.